Jumapili, Februari 23, 2014

TIMBULO HOI KWA PENZI LA SKYNER

CHIPUKIZI wa Bongo Fleva, Ally Timbulo amefunguka kuwa alimwagana na mwigizaji Skyner Ally ‘Skaina’ kwani aligundua kuwa ana uhusiano na Mbongo Fleva mwenzake, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
Timbulo alisema ishu hiyo ilitokea miaka kadhaa iliyopita ambapo ‘alimsarendia’ mlimbwende huyo ili awe mpenzi wake na aliposhtuka kuwa ana uhusiano na Nay wa Mitego, fasta alibadili uelekeo.
“Daah! Nilipogundua ana uhusiano na Nay, fasta nilimpotezea,” alisema Timbulo, alipotafutwa Skaina, alisema: “Usiniulize hizo habari, ulivyosikia ndiyo hivyohivyo.”

0 comments:

Chapisha Maoni