Jumamosi, Februari 08, 2014

MVUA KUBWA YAEZUA PAA LA MAJENGO YA SHULE YA SEKONDARI

Mvua iliyoambatana na upepo mkali imeezua  shule ya  sekondari Kondoa Islamic iliyoko wilayani Kondoa mkoani Dodoma na kusababisha wanafunzi  33 kukimbizwa hosipitali  huku wengine zaidi ya 100 wakikosa  mahala pa kulala pamoja na kuharibu vitu mbalimbali ikiwemo vifaa vya kufundishia na kujifunzia vyakula na malazi ya wanafunzi.
Chanzo kilifika eneo la shule na kushuhudia uharibifu mkubwa uliofanywa na mvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali ambapo sehemu zilizoathirika kwa kiasi kikubwa ni pamoja na bweni la wasichana, ukumbi wa kufanyia mitihani, madarasa pamoja na baadhi ya ofisi huku baadhi ya wanafunzi wakionekana kuhaha kutafuta sehemu za kujistiri kufuatia vitanda na matandiko yao kulowana na maji huku mvua ikiendelea kuwanyeshea .
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Salum Athumani anasema mvua hiyo imeathiri utendaji wa shule hiyo kwa kiasi kikubwa kutokana na kusimamisha masomo  ya wanafunzi huku akiwaomba wakazi wa wilaya hiyo na wilaya za jirani kutoa msaada wa hali na mali kuhakikisha hali ya shule hiyo inarejea kama ilivyokuwa awali.
Kufuatia janga hilo uongozi wa halmashauri ya wilaya ya kondoa kupitia kamati ya maafa ya wilaya umechukua hatua za dharura ikiwemo kupeleka vifaa vya ujenzi kwa ajili ya kufanya ukarabati ambapo mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya kondoa ezekiel mwalongo amesema licha ya mvua hiyo kuleta madhara shuleni hapo lakini pia imeezua zahanati ya kijiji cha Mkekena kata ya Itololo pamoja na nyumba tatu za wakazi wa kijiji hicho.

0 comments:

Chapisha Maoni