Jumatano, Februari 19, 2014

BABY MADAHA SASA MUZIKI, FILAMU BASI!!!

IKIWA imepita miezi kadhaa tangu anaswe katika mtego  wa kujiuza na makachero wa OFM ya Global Publishers, staa wa Bongo, Baby Madaha ametangaza kuachana na sanaa ya muziki na filamu kwa maelezo kuwa amechoshwa na  maisha ya presha.
Akistorisha na paparazi wetu juzikati jijini Dar es Salaam, Madaha alisema ishu ile imemsababishia matatizo makubwa ya kifamilia na hata kibiashara, hivyo kujutia mchezo mzima ulivyokuwa.
Alisema filamu anayoisambaza kwa sasa na kibao chake cha mwisho kukitoa cha Mr. Dj ndizo zitakazofunga pazia la mambo ya sanaa kwa upande wake.
SOURCE: GPL

0 comments:

Chapisha Maoni