Huko Singida watu wenye hasira
walilichoma moto basi la Kampuni ya Mtei Express ya mjini Arusha, baada
ya kulituhumu kuhusika katika ajali ya kuigonga pikipiki na kuua watu
watatu wa familia moja.
Watu hao ni Tamili Shaban na Kassimu ambao
walifariki papo hapo kwenye eneo la tukio ambalo ni kitongoji cha
Ijanuka kijiji cha Kisasida Manispaa ya Singida.Hamza amefariki dunia
akiwa anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa mjini hapa.
Miili ya watu hao imehifadhiwa.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Singida, SACP,Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lililitokea jana saa moja na dakika moja asubuhi huko katika Kitongoji cha Ijanuka Kijiji cha Kisasida.
Alisema siku ya tukio, basi la Kampuni ya Mteni
lenye namba za usajili T.742 ACU aina ya scania likiendeshwa na Dismas
Ludovick, lilikuwa linatokea Singida mjini likielekea Arusha mjini.
Kamwela alisema lilipofika Kitongoji cha Ijanuka,
pikipiki iliyokuwa inaendeshwa na Shaban Bunku huku akiwa amepakia
watoto wake watatu, ilikatisha ghafla kitendo kilichosababisha kugongwa
na kuburutwa kwa hatua 20.




0 comments:
Chapisha Maoni