Mdhamini wa klabu ya Yanga, Mama Fatuma
Karume amesema Yanga hawajakurupuka kukacha michuano ya Mapinduzi ila
wana sababu zao za msingi na ndiyo maana wamefanya hivyo.
Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwake Mahisara
jana, Mama Karume alisema Yanga siyo wajinga kuamua kujitoa kwenye
michuano hiyo, ambapo badala ya watu kuwalaumu walitakiwa waulize sababu
za Yanga kujitoa.
“Yanga hawajakataa Mapinduzi, Mapinduzi ni ya
Serikali, nina hakika kabisa Yanga hawajakataa haya Mapinduzi,
walichokikataa ni michezo ya mapinduzi, na wana sababu zao, hao
waandaaji wameona Yanga wamejitoa mara tatu mfululizo kwa nini
wasiwatafute Yanga wakakaa chini na kuyamaliza?”alihoji Mama Karume.
Alisema, “Hata siku moja waandaaji wa michuano ya
mapinduzi hawajawahi kunifuata hapa wakaniambia habari za Yanga na hapa
wanapajua viongozi chungu mbovu wa michezo wa Dar na Zanzibar
wananifahamu, wangekuja kwangu mimi lazima ningewaita Yanga niwaulize
kulikoni, lakini wao hawajafanya hivyo.”
Mama Karume alisema, “Najua kama Yanga wamejitoa
na mwaka jana walileta watoto waandaaji wakawafukuza, sasa wangenifuata
tukakaa na Yanga tukazungumza, Yanga si wajinga eti kujitoa, kwani mtu
hakatai kunywa maji kama hayamdhuru, ukiona kakataa basi jua
yanamdhuru.”
“Wao mwaka wa kwanza wamejitoa, wakapiga makelele
kwenye vyombo vya habari ikapita, mwaka wa pili wamejitoa, mwaka wa tatu
wameleta vitoto mkawafukuza, hamjiulizi tu kuna kitu gani mkakaa chini
kuzungumza?”alihoji Mama Karume.



0 comments:
Chapisha Maoni