Jumapili, Februari 25, 2018

MATUMIZI SAHIHI YA GIA D, L, 2, 3 NA O/D KATIKA GARI AMBAZO NI AUTOMATIC

Fichuo inafahamu kuwa yawezekana wewe ni moja ya watu wanaopata shida katika matumizi ya GIA Automatic, kwanza ujue kabisa katika hali ya kawaida gari yako inapaswa kuwa katika D kwa maana ya Drive na hii inategemeana na mazingira ya barabara na hali yali ya hewa kama ni nzuri lakini 2, 3 hutumika tu pale unapokuwa ama unashuka mteremuko mkali au unapanda mlima mkali kama vile Sekenke na unataka ushuke au upande kwa speed ile ile ila isizidi 40/60 hapo ndipo unashauriwa kutumia 2, 3
Namba 2, 3 na L huwa inalock GEAR BOX ili gear zisibadilike (-/+) kama ambavyo zinabadika ukiweka D na itambulike kuwa unaweza kubadili toka D kwenda 2 au 3 wakati wowote gari inapokuwa katika mwendo ila hakikisha usiwe speed zaidi ya 40/60 maana kinachofanyika ni kwamba D inasababisha sahani DISKS zilizomo ndani ya GEARBOX kufanya kazi na hii hupelekea ile hydrolic iliyomo kupata joto linalotoka katika zile sahani ambalo joto lile husababisha GEARBOX kutokuwa na nguvu ile ile (constant velocity) na ndo maana ukiweka 2, 3 au L gear box inakuwa kwenye lock na sahani hazisuguani maana inakuwa inatumika sahani/disk moja tu kwa hiyo inasaidia ile hydrolic kupoa pia na ndo maana gari huongeza nguvu kwa ghafla.
Image result for automatic transmission L inatumika pale unapokuwa either umekwama au unavuta gari jingine au tera ila inapaswa itumike kwa muda mfupi sana maana inanguvu sana na pia inaongeza ulaji wa mafuta, kwahiyo kama ukitoka katika mkwamo na unaona bado barabara si nzuri labda utelezi au unavuta mzigo kwa mwendo mrefu basi unaweka 2 au 3 na wakati huohuo unaweza kuweka hata D kama hali ya njia na mzigo vinaruhusu na unaweza kuongeza walau speed 40/60 au zaidi kama utaweka D kwa maana rahisi zaidi ni kwamba 2,3,na L inafanya kazi kama gari ya Manual na hii inakuwa rahisi kwa yeyote ambaye anafahamu kuendesha manual.
Image result for car on mud Over Drive inatumika pale gari inapokuwa speed zaidi ya 60/80 kutegemeana na aina ya gari na hili hutokea bila wewe kujua maana gari yenyewe  hufanya hivyo ndio maana unashauriwa iwe ON muda wote kusudi gari ichague ni wakati gani iweke ON/OFF maana ukiwa chini ya speed 60/80 hata kama umeweka ON bado inakuwa haifanyi kazi.
Mwisho ni kwamba OD unaweza kuitumia kama break/stop engine hasa unapokuwa zaidi ya Speed 80 na wakati huo iko ON yaani katika dashboard taa ya OD izime...ikiwaka maana yake iko OFF, basi ili upunguze mwendo kwa haraka unachofanya ni kuweka OFF na wakati huo unakanyaga break taratibu utaona mwenyewe gari lako linavyopunguza mwendo taratibu na wakati mwingine si lazima ukanyage break, we iweke OFF tu halafu toa mguu katika pedal ya mafuta gari lazima li slow down na kama lilikuwa ni tuta na umeshalipita basii iweke tena ON ongeza mafuta au unaweza kuweka 2 au 3 ili gari ianze kwa kasi zaidi na ikiisha changanya basi rudi kwenye D na endelea kama kawaida.

2 comments: