Ijumaa, Mei 12, 2017

THE ROCK ANAUTAKA URAIS WA MAREKANI 2021

Aliyekuwa nyota wa mchezo wa miereka Marekani Dwayne Johnson maarufu 'The Rock' anataka kuwania urais nchini humo.
Katika mahojiano na jarida la GQ, nyota huyo wa uigizaji anasema kuwa amelifikiria sana wazo hilo.
Anasema kwamba iwapo angekuwa rais ingekuwa muhimu.
''Uongozi ni muhimu. Kuchukua jukumu la kila mtu''.
Lakini Johnson sio nyota pekee mwenye maono ya kutaka kuhamia katika ikulu ya Whitehouse 2021.
Mark Zuckerberg , bilionea na mkurugenzi wa mtandao wa facebook pia huenda ana ndoto kama hiyo.
Amekuwa na mpango wa kuwatembelea raia wote wa Marekani katika majimbo 50 na amekuwa akipeperusha hewani ziara zake moja kwa moja katika mtandao wa facebook hatua ambayo inaokena kuupigia debe mtandao huo.

0 comments:

Chapisha Maoni