Jumatatu, Machi 13, 2017

UKATA WAIONDOA MALAWI KOMBE LA MATAIFA AFRIKA 2019

Malawi imetangaza kwamba imejiondoa kutoka kwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2019 pamoja na michuano ya Ubingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani ya 2018.
Taifa hilo limechukua hatua hiyo kutokana na matatizo ya kifedha pamoja na kukosa mkufunzi wa timu ya taifa.
Shirikisho la Soka la Malawi lilitoa taarifa baada ya kunyimwa idhini ya kumwajiri kocha kutoka nje na serikali ya nchi hiyo.

0 comments:

Chapisha Maoni