Jumapili, Machi 26, 2017

CNN YASHUKIWA

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa televisheni ya CNN ya Marekani imekuwa chombo cha kueneza propaganda za kisaisa za nchi hiyo.
Maria Zakharova amekosoa habari za kichochezi zinazotangazwa na televisheni ya CNN ya Marekani na kusema yanayojiri Marekani yanaonesha jinsi vyombo vya habari vinavyoshiriki katika michezo ya kisaisa, mashinikizo na kutoa vitisho.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ameongeza kuwa, televisheni ya CNN ilipoteza hadhi na uaminifu wake mbele ya walimwengu muda mrefu uliopita.
Kuhusu madai ya televisheni ya CNN kwamba Rais Vladmir Putini aliafikiana na Donald Trump juu ya kutoa pigo dhidi ya Hillary Clinton katika uchaguzi uliopita wa Rais wa Marekani, Maria Zakharova amesema kuwa, katika kampeni zake za uchaguzi, mgombea aliyeshindwa wa chama cha Democratic alisema: Inasikitisha kuona kwamba CNN imebadilika na kuwa chombo kilichochuja.
Televisheni ya CNN ambayo katika kipindi cha kampeni za uchaguzi wa Rais wa Marekani ilituhumiwa kumuunga mkono na kumpigia debe Hillary Clinton, imekuwa ikimkosoa vikali Rais wa sasa wa nchi hiyo, Donald Trump na kumtuhumu kwamba alikuwa na uhusiano na ushirikiano wa siri na Rais Vladmir Putin wa Russia. 

0 comments:

Chapisha Maoni