Jumatano, Septemba 03, 2014

EBOLA KUFANYIWA MKUTANO

Shirika la afya Ulimwenguni WHO limeandaa mkutano wa siku mbili unaoanza leo Geneva Uswis ukilenga kujadili uwezekano wa matibabu dhidi ya ugonjwa wa Ebola.
Dawa zote zenye uwezekano wa kutibu ugonjwa huo zitajadiliwa na kufanyiwa uchunguzi wa kina wa maoni ya kitaalam.
Hata hivyo shirika la misaada la dawa MSF limeonya kuwa huenda mkutano huo ukashindwa kuwa na matokeo makubwa katika mlipuko wa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi ambako watu 1900 wamefariki kutokana na ugonjwa huo.
Mkuu wa shirika hilo la MSF Brice de la Vigne akikosoa kuhusiana na mkutano huo amesema kuwa kilichopaswa kutiliwa mkazo kwa sasa na mashirika ya kimataifa ni kuongeza idadi ya hospitali dharula katika maeneo ya milipuko ya Ebola.

0 comments:

Chapisha Maoni