Jumatatu, Juni 23, 2014

MWANAMKE MSUDAN ALIYEHIUKUMIWA KIFO NA VIBOKO 100 KWA KOSA LA KUOLEWA NA MKRISTO AACHILIWA HURU NA MAHAKAMA

Mahakama nchini Sudan imemuachilia huru mwanamke aliyehukumiwa kifo mwezi uliopita kwa kuasi imani yake ya Kiislam. Kesi ya Meriam Ibrahim ilisababisha shutuma nyingi kimataifa. Alihukumiwa pia mikwaju mia moja kwa kile mahakama ilitaja kuwa ni uzinzi kwa kuolewa na Mkristo. Alijifungua mtoto wa kike akiwa gerezani.

0 comments:

Chapisha Maoni