Wanawake/wanaume wengi hawafahamu
wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia
sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia
kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.
PILI-
Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke
unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke
unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii
inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.
TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni
kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao
ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako
hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.
NNE -
Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa
suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi
unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya
kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na
makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.
Katika uchunguzi huu
mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha
huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka
alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza
amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila
kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.
TANO - Ajipe muda wa
kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha
aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi
mwanaume huyo alivyopata au kukosa.
Ikibainika mwanaume
aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa,
basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia
kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.
Lakini angalizo
kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika
kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni
mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni
vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.
SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya
kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao.
Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na
wanapokwenda.
Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime
umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda
kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri
usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na
mara zote wasaidiane kwa ukaribu.
0 comments:
Chapisha Maoni