Jumapili, Aprili 06, 2014

ABBAS AMETUPILIA MBALI PENDEKEZO LA JOHN KERRY

Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas ametupilia mbali pendekezo lililotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry la kutojiunga na mikataba ya kimataifa.

Mmoja wa maafisa wa Palestina leo ameripoti kuwa Mahmoud Abbas amekataa pendekezo lililotolewa na John Kerry kwamba taifa la Palestina liache kujiunga na makubaliano na mikataba ya kimataifa kwani litazidisha hasira ya Israel. Afisa huyo amesema kwamba Abbas kupitia njia ya simu amemsisitizia John Kerry kuwa, hatoacha kufuatilia suala hilo kwani si takwa kubwa kwa Wapalestina na kwamba hawatotishwa na vitisho vya Israel.
Maafisa wa Palestina wiki hii waliamua kutuma maombi katika Umoja wa Mtaifa ili kujiunga na mikataba 13 ya kimataifa, ikiwa ni baada ya Israel kukataa kuwaachilia huru mateka wa Kipalestina kama walivyokuwa wamepatana.

0 comments:

Chapisha Maoni