Jumanne, Januari 14, 2014

WATU WAWILI WAFARIKI KATIKA AJALI YA BODA BODA BAADA NA SCANIA



Tarehe 13.01.2014 Majira Ya Saa 04:30hrs Huko Katika Eneo La Sae, Kata Ya Mwakibete, Tarafa Ya Iyunga, Jiji Na Mkoa Wa Mbeya Barabara Ya Mbeya/Njombe. Pikipiki T.436 Clp Aina Ya T-Better Ikiendeshwa Na Gabriel  Ngalele, Miaka 24, Kyusa, Mkazi Wa Uyole   Iligonga Kwa Nyuma Gari T.684 Bvy Aina Ya Scania Lililokuwa Limeegeshwa Na Dereva Asiyefahamika Jina Wala Makazi Yake Na Kusababisha Kifo Cha Mwendesha Pikipiki Huyo Pia Kusababisha Kifo Kwa Abiria Aliyekuwa Katika Pikipiki Hiyo Ambaye Hafahamiki Jina Wala Makazi Yake Jinsi Ya Kike. 
Chanzo Cha Ajali Kinachunguzwa. Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi Wa Polisi Ahmed Z. Msangi Anatoa Wito Kwa Madereva Kuwa Makini Wanapotumia Vyombo Vya Moto Kwa Kuzingatia Sheria Na Alama Za Usalama Barabarani Ili Kuepuka Ajali Zinazoweza Kuepukika.

0 comments:

Chapisha Maoni