Jumanne, Januari 14, 2014

PINDA ANAKWENDA KUMALIZA MGOGORO KITETO LEO

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda leo anakwenda Wilaya ya Kiteto, Arusha kutafuta suluhu ya mapigano baina ya wakulima na wafugaji katika Hifadhi ya Embroi Murtangosi yaliyosababisha vifo vya watu 10.
Mwandishi wa Habari wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Irene Bwire alisema jana: “Ni kweli Waziri Mkuu atakwenda kutembelea wilayani Kiteto ili kuongoza juhudi za kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.”

0 comments:

Chapisha Maoni