Jumatano, Januari 15, 2014

OFISI YA RAIS RWANDA YAKADHIBISHA KIFO CHA RAIS KAGAME

Ofisi ya Rais wa Rwanda imekadhibisha vikali uvumi ulioenea nchini humo na nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwamba Rais Paul Kagame wa nchi hiyo amefariki dunia.
Taarifa zinasema kuwa, uvumi wa habari za kufariki dunia Rais Kagame, umeamsha furaha hasa kwa wakazi wa miji ya mpaka wa nchi hiyo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mara kadhaa Rwanda imekuwa ikituhumiwa kwa kuingilia kijeshi katika maeneo ya mpaka na Kongo.
Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulitoa taarifa na kuituhumu tena serikali ya Kigali kwa kuyaunga mkono makundi yanayobeba silaha na hasa waasi wa zamani wa M23 waliokuwa mashariki mwa Kongo. Hata hivyo ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa imekosolewa vikali na serikali ya Rwanda.
Rais Paul Kagame mwenye umri wa miaka 56 alichukua madarakani mwaka 1994 baada ya kutokea mauaji ya kimbari yaliyopelekea watu wasiopungua laki nane hasa wa kabila la Kitutsi kuuawa nchini humo.

0 comments:

Chapisha Maoni