Jumatatu, Januari 20, 2014

MTOTO WA KIMASAI AUAWA KWA KUPIGWA FIMBO KICHWANI

Tarehe 19.01.2014 Majira Ya Saa 11:00 jioni Huko Katika Kijiji Na Kata Ya Itamboleo, Tarafa Ya Ilongo, Wilaya Ya Mbarali Na Mkoa Wa Mbeya, Mtoto Lumiki Rahim, Miaka 06, Mmasai, Mwanafunzi Shule Ya Msingi Kapunga Darasa La Kwanza Aliuawa Kwa Kupigwa Na Fimbo Kichwani Na Mtoto Bedon Said, Miaka 12, Muwanji, Mwanafunzi Shule Ya Msingi Kapunga Darasa La Sita. Chanzo Kinachunguzwa. Mwili Wa Marehemu Umehifadhiwa Hospitali Ya Misheni Chimala Kwa Uchunguzi Wa Kitabibu. Mtuhumiwa Amekamatwa. Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi Wa Polisi Ahmed Z. Msangi Anatoa Wito Kwa Wazazi/Walezi Kudumisha Malezi Bora Kwa Watoto Wao Wangali Wadogo Ili Wakue Katika Misingi Na Ustawi Mzuri Wa Jamii Na Kujiepusha Na Vitendo Vya Uhalifu.

0 comments:

Chapisha Maoni