Ijumaa, Novemba 08, 2013

NYAMA KATIKA MACHINJIO DAR ES SALAAM SI SALAMA

Afya za maelfu ya walaji wa  nyama katika Jiji la Dar es Salaam zipo hatarini baada ya kubainika kuwa nyama inayochinjwa katika machinjio mengi haifai kwa matumizi ya binadamu.
Hali hiyo inatokana na mifugo kuchinjwa bila kufuata taratibu za afya na kuingizwa sokoni, ikiwamo nyama hizo kutokaguliwa na wataalamu wa mifugo kabla ya kuchinjwa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika machinjio mbalimbali ya maeneo ya Vingunguti, Ukonga, Kimara Suka, Tegeta na Mbagala, umebaini taratibu za kuchinja hazifuatwi huku maeneo hayo yakiwa yamejaa uchafu.
Mwandishi wa habari hizi alifika katika machinjio hayo kwa nyakati tofauti alfajiri na kushuhudia ukiukwaji wa taratibu za uchinjaji, ambapo nyama zinatupwa ovyo, kwenye mazingira hatari, huku nyingine zikiwekwa karibu na  madimbwi ya maji machafu.

0 comments:

Chapisha Maoni