Serikali ya Zambia imeunga mkono tangazo la kupiga marufuku
uuzwaji wa pombe kali zilizofungwa kwenye vikaratasi vya nailoni
maarufu kama viroba.
Hivi karibu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro ,
kwa niaba ya Kamati ya Ulinzi na Usalama, alipiga marufuku uuzwaji wa
pombe kutoka Zambia na Malawi akisema zinaharibu nguvu kazi na
kusababisha kero nyingi kwa vijana.
Pombe hizo za viroba zilizopigwa marufuku ni pamoja na; Double Punch, Power No 1, Boss, Royal Punch na Charger.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais wa Jimbo la Muchinga
nchini Zambia, Charles Sipanje akiwa jijini Mbeya juzi, alisema pombe
hizo, zilishapigwa marufuku kutengenezwa nchini mwao.
Sipanje alisema, viroba hivyo maarufu kwa jina la
‘Tujilinjili’ nchini Zambia, vinauzwa Tanzania baada ya watengenezaji
wake kupata soko la nje.
“Sisi tunaruhusu pombe za aina hiyo ziwe kwenye
chupa kubwa na siyo karatasi. Hivyo ni halali kwa viongozi wa Mbeya
kupiga marufuku,’’ alisema.
Pombe kali zilizofungwa kwenye karatasi hizo
zinadaiwa kuuzwa kwa kati ya Sh100 na Sh 700, jambo linalosababisha
watu wengi, wakiwamo watoto na madereva kunywa bila kuzingtia taratibu
na sheria za nchi.
Tayari vifo kadhaa vinavyodaiwa kusababishwa na
pombe za aina hiyo vimeripotiwa, kikiwamo cha hivi karibuni ambapo mtu
mmoja alifariki baada ya kunywa pombe nyingi kwenye mkesha wa Mbio za
Mwenge, wilayani Rungwe.



0 comments:
Chapisha Maoni