Habari
toka kwa maafisa wa polisi zinaeleza kuwa waliouawa ni mwanamke aliyetambulika
kwa jina moja la Sophia anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 35-40, Msafwa,
mkulima na mkazi wa Ituha pamoja na mwanaume ambaye hajatambulika aneyekadiriwa
kuwa na umri wa miaka 40-45.
Taarifa
zinaeleza kuwa wawili hao wamefariki dunia wakati wakiwa njiani kupelekwa
hospitalini baada ya kushambuliwa kwa kupigwa mawe na marungu sehemu mbali
mbali za miili yao na mtu/watu wasiojulikana ambao waliwavamia wakiwa njiani kurejea nyumbani usiku huo.
Aidha
chanzo cha mauaji hayo kimetajwa kuwa ni wivu wa kimapenzi na mpaka sasa mtu
mmoja aliyefahamika kwa jina la Zebedayo John, 32, Msafwa, mkulima na mkazi wa
Ituha tayari anashikiliwa na jeshi la
polisi baada ya kutiliwa shaka kuhusika na tukio hilo lakini upelelezi bado
unaendelea.
Pamoja na
hayo kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya,
kamishna msaidizi wa jeshi la polisi Diwani Athumani anatoa wito kwa jamii
kuacha kujichukulia sheria badala yake watumie njia za mazungumzo kumaliza
migogoro yao. Vile vile ametoa rai kwa yeyote aliye na taarifa juu ya waliko
wahusika wa tukio hilo wazitoe ili wakamatwe na sheria ichukue mkondo wake.
0 comments:
Chapisha Maoni