Jumapili, Agosti 04, 2013

BALOZI ZAFUNGWA MAREKANI

Ofisi zaidi ya 12 za mabalozi wa Marekani katika Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini zimefungwa.

Hatua hiyo inafuatia serikali ya Marekani kusema Ijumaa kwamba inaamini kuwa al-Qaeda au kundi linaloshirikiana na al-Qaeda huenda likawa linapanga mashambulio.
Ubalozi wa Marekani mjini Kabul piya umefungwa kwa sababu ya ilani hiyo kuhusu usalama.
Mataifa kadha ya Ulaya nayo yamefuata - Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zimesema kuwa balozi zao mjini Sanaa, Yemen, zitafungwa mwisho wa juma.

0 comments:

Chapisha Maoni