Ijumaa, Aprili 01, 2016

ALIYEMTISHIA KIFO RAIS MAGUFULI AFIKISHWA MAHAKAMANI

Kijana Hamimu Seif, mkazi wa Mwananyamala Ujiji, Dar es Salaam, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kumtishia kifo Rais John Magufuli.
Mbele ya Hakimu Mkazi Helleni Liwa, Keneth Sekwao, Wakili wa Serikali, aliiambia mahakama kuwa kijana huyo alitishia kumuua rais Machi 10 mwaka huu, alipokuwa katika baa ya Soweto maeneo ya Makumbusho, Jijini Dar es Salaam.
Sekwao ameeleza mahakama kuwa kijana huyo alitamka kuwa amechoshwa na mambo anayofanya rais, na kwamba yupo tayari kujitoa mhanga kwa kujilipua na bomu.
Mshitakiwa amekana mashitaka, na mahakama imeweka wazi dhamana yake.
Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo tarehe 14 Aprili mwaka huu.

0 comments:

Chapisha Maoni