Jumapili, Februari 07, 2016

MAMENEJA WA TANESCO KIKANDA SASA KUTUMBULIWA MAJIPU YAO

Taarifa tuliyoipata hivi sasa ni kwamba kutakuwa na tathini ambazo watakuwa wakifayiwa mameneja wa shirika la umeme Tanzania TANESCO wale wa kanda zote zilizopo Tanzania. Na katika tathini hiyo vigezo vitakavyotumika kuwaondoa au kuwabakiza kwenye nafasi zao ni hizi:

(1) Ongezeko la ubora wa huduma za upatikanaji wa umeme 
(2) Ongezeko la wateja wapya 
(3) Ongezeko la ukusanyaji wa mapato (fedha). 
(4) Ubunifu, ufanisi na umakini kiutendaji.

NI jukumu lao kuwataja wafanyakazi wa TANESCO wanaowakwamisha kiutendaji.
Tathmini ya Desemba - Februari itafanyika 1.3. 2016.

0 comments:

Chapisha Maoni