Ijumaa, Januari 15, 2016

KIFO CHA RAIS KABILA

Siku kama ya leo miaka 15 iliyopita Rais Laurent Desire Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alipigwa risasi na mmoja wa walinzi wake katika ikulu ya Rais na kujeruhiwa vibaya. Baada ya tukio hilo kulienea habari za kutatanisha juu ya hatima ya Rais huyo. Tarehe 18 Januari yaani siku mbili baadaye, serikali ya Kinshasa ilithibitisha kufariki dunia Rais huyo. Kabila alizaliwa mwaka 1939 huko Katanga alihudhuria masomo ya Chuo Kikuu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Tanzania. Aliingia madarakani mwaka 1997 baada ya vikosi alivyokuwa akiviongoza kuuteka mji wa Kinshasa, na kupelekea Rais Mobutu Sese Seko kukimbilia nje ya nchi. Tarehe 26 Januari Joseph Kabila mwana wa Rais Kabila alishika haramu za uongozi nchini Congo.

0 comments:

Chapisha Maoni