Jumatano, Oktoba 22, 2014

AMUUA BINTI YAKE KWA MAWE BAADA YA KUFANYA MAPENZI KABLA YA NDOA

Mfuasi mmoja wa kundi la ISIS la Syria ameungana na wanajeshi kadhaa wa kundi hilo kufanya mauaji ya kinyama kwa kumpiga mawe binti yake wa kumzaa hadi kufa baada ya kugundulika kuwa alizini.
Kundi la ISIS limeachia video inayoonesha tukio hilo la kusikitisha linaloelezwa kufanyika katika jiji la Hama nchini Syria.
Katika video hiyo iliyoripotiwa pia na mtandao wa Mirror wa Uingereza, msichana huyo anaonekana mnyonge akimuomba msamaha baba yake, 
tafadhali baba….nisamehe.
Lakini baba yake anasikika akisema, 
mimi sio baba yako tena.
Aliongeza kuwa anatumaini adhabu anayompa binti yake itakuwa fundisho kwa wanawake wengine.
Baba huyo alioenekana akiwageukia wapiganaji wa ISIS na kuwapa ishara kuwa adhabu ianze, na mwisho yeye anaonekana akiwa na jiwe kubwa zaidi lililoutoa uhai wa binti yake.

0 comments:

Chapisha Maoni