Alhamisi, Oktoba 30, 2014

AJALI YA TRENI LEO VINGUNGUTI

Gari moshi(treni) limeacha njia yake na kuanguka kuhu likiwa limebeba mabehewa Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Taarifa zina bainisha kuwa njia hiyo ya Treni ni mbaya kwa kuchimbika chimbika nahivyo kusababisha mkwamo kwenye treni hiyo na hivyo kulazimika kuanguka huku tairi zake kuchomoka na kila moja kuwa upande wake.
Katika msemo wa kufa kufaana panapo tokea ajali,iliweza kuwalazimu askari wa kutuliza ghasia kufika mara moja eneo hilo la vingunguti kwa lengo lakuweka ulinzi dhidi ya wanaoweza kutia hasara kwa kuondoka na bhaadhi ya vyuma kwenye treni hiyo.
Mashuhuda wa walioshuhudia ajali wanasema kuwa njia ya treni hiyo si salama sana,na hivyo njia kupelekea hadi kuanguka na wataalamu wanasema Pin Lock ndio iliyo sababisha pia kuweza kushindwa treni kukaa kwenye njia yake baada ya kukatika. Haijafahamika Mabehewa yalikuwa na nini ndani yake.

0 comments:

Chapisha Maoni