Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anataka
kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, huku pauni milioni
14 ikidhaniwa kutosha kufanikisha uhamisho wake (Sunday Express),
Arsenal wapo tayari kupambana na Manchester United kumwania beki wa
Borussia Dortmund Mats Hummels, 25, kwa kutoa pauni milioni 30 (Sunday
Mirror), Manchester United wanakabiliwa na wakati mgumu kumsajili winga
wa Real Madrid, Angel Di Maria, 26,kufuatia Bayern Munich pia kumtaka
mchezaji huyo (Sunday Times), Tottenham wanajiandaa kutaka kumsajili
Samuel Eto'o aliyekuwa Chelsea msimu uliopita (Sun), mwenyekiti wa
Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge amesema klabu yake "haina haraka"
kumsajili Marco Reus, 25, wa Borussia Dortmund, ambaye anafuatiliwa na
Manchester United na Liverpool (Sunday Express), meneja wa Swansea Gary
Monk amesema mshambuliaji wake Wilfried bony, 25, haondoki, licha ya
Liverpool kumuulizia (Talksport), hata hivyo Tottenham wanamtaka pia
Bony na vilevile kiungo Morgan Schneiderlin wa Southampton, na wawili
hao huenda wakagharimu pauni milioni 45 (Sunday Mirror), Real Madrid
huenda wakamchukua kipa wa Chelsea Petr Cech, iwapo Thibault Cortois,
22, atakuwa namba moja Darajani (Sunday Telegraph), mshambuliaji wa
Manchester City john Guidetti, 22 aliyekuwa kwa mkopo Feyenoord, huenda
akajiunga na Ajax, kwa kuwa hahitajiki Etihad (Mail on Sunday), meneja
wa Aston Villa Paul Lambert atakuwa na mazungumzo na beki Ron Vlaar, 29
baada ya Juventus kutaka kumsajili (Sun), beki wa Atlètico Madrid,
Javier Manquillo, 20 anajiandaa kufanya vipimo vya afya Liverpool
kukamilisha uhamisho wa mkopo wa miaka miwili (Liverpool Echo),
mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie, 30, atakosa kucheza
mwanzo wa msimu akiendelea kupumzishwa baada ya Kombe la Dunia (Sunday
People), meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema "alishangazwa" na
magoli manne ya Yaya Sanogo wakati Gunners waliposhinda 5-1 dhidi ya
Benfica katika Kombe la Emirates (Mail on Sunday), meneja wa Chelsea
Jose Mourinho amesema Frank Lampard, 36, ambaye atajiunga na Manchester
City kwa mkopo, kutoka New York City FC, na Ashley Cole, 33, aliyejiunga
na Roma, wote walipewa mikataba mipya Darajani (Daily Star), Thomas
Vermaelen atasaini mkataba na Barcelona kutoka Arsenal. Louis van Gaal
alikuwa akimtaka beki huyo, lakini atasaini mkataba wa pauni milioni 10
(Daily Mirror), Arsenal wanakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa
Sporting Lisbon, William Carvalho (Daily Star).
0 comments:
Chapisha Maoni