Jumapili, Agosti 03, 2014

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI YA LEO

Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anataka kumsajili mshambuliaji wa AC Milan Mario Balotelli, huku pauni milioni 14 ikidhaniwa kutosha kufanikisha uhamisho wake (Sunday Express), Arsenal wapo tayari kupambana na Manchester United kumwania beki wa Borussia Dortmund Mats Hummels, 25, kwa kutoa pauni milioni 30 (Sunday Mirror), Manchester United wanakabiliwa na wakati mgumu kumsajili winga wa Real Madrid, Angel Di Maria, 26,kufuatia Bayern Munich pia kumtaka mchezaji huyo (Sunday Times), Tottenham wanajiandaa kutaka kumsajili Samuel Eto'o aliyekuwa Chelsea msimu uliopita (Sun), mwenyekiti wa Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge amesema klabu yake "haina haraka" kumsajili Marco Reus, 25, wa Borussia Dortmund, ambaye anafuatiliwa na Manchester United na Liverpool (Sunday Express), meneja wa Swansea Gary Monk amesema mshambuliaji wake Wilfried bony, 25, haondoki, licha ya Liverpool kumuulizia (Talksport), hata hivyo Tottenham wanamtaka pia Bony na vilevile kiungo Morgan Schneiderlin wa Southampton, na wawili hao huenda wakagharimu pauni milioni 45 (Sunday Mirror), Real Madrid huenda wakamchukua kipa wa Chelsea Petr Cech, iwapo Thibault Cortois, 22, atakuwa namba moja Darajani (Sunday Telegraph), mshambuliaji wa Manchester City john Guidetti, 22 aliyekuwa kwa mkopo Feyenoord, huenda akajiunga na Ajax, kwa kuwa hahitajiki Etihad (Mail on Sunday), meneja wa Aston Villa Paul Lambert atakuwa na mazungumzo na beki Ron Vlaar, 29 baada ya Juventus kutaka kumsajili (Sun), beki wa Atlètico Madrid, Javier Manquillo, 20 anajiandaa kufanya vipimo vya afya Liverpool kukamilisha uhamisho wa mkopo wa miaka miwili (Liverpool Echo), mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie, 30, atakosa kucheza mwanzo wa msimu akiendelea kupumzishwa baada ya Kombe la Dunia (Sunday People), meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema "alishangazwa" na magoli manne ya Yaya Sanogo wakati Gunners waliposhinda 5-1 dhidi ya Benfica katika Kombe la Emirates (Mail on Sunday), meneja wa Chelsea Jose Mourinho amesema Frank Lampard, 36, ambaye atajiunga na Manchester City kwa mkopo, kutoka New York City FC, na Ashley Cole, 33, aliyejiunga na Roma, wote walipewa mikataba mipya Darajani (Daily Star), Thomas Vermaelen atasaini mkataba na Barcelona kutoka Arsenal. Louis van Gaal alikuwa akimtaka beki huyo, lakini atasaini mkataba wa pauni milioni 10 (Daily Mirror), Arsenal wanakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa Sporting Lisbon, William Carvalho (Daily Star).

0 comments:

Chapisha Maoni