Jumatano, Agosti 13, 2014

TAREHE YA LEO KATIKA HISTORIA

Siku kama ya leo miaka 54 iliyopita, Jamhuri ya Afrika ya Kati ilijikomboa na kupata uhuru toka kwa mkoloni Mfaransa. Ilikuwa katikati ya karne ya 19 wakati nchi hiyo iliyokuwa ikijulikana hapo kabla kwa jina la Ubangi-Shari, ilipounganishwa na makoloni ya Ufaransa barani Afrika. Hata hivyo mwaka 1958, Jamhuri ya Afrika ya Kati ilijipatia Mamlaka ya Ndani na miaka miwili baadaye yaani mwaka 1960, ikajikomboa na kupata uhuru kamili.
Katika siku kama ya leo miaka 36 iliyopita kulingana na kalenda ya Hijria Shamsiya, maandamano makubwa yalifanyika katika mji wa Esfahan nchini Iran, baada ya kupamba moto harakati za mapambano za wananchi Waislamu dhidi ya utawala wa Shah. Kwa utaratibu huo, wananchi wa mji huo waliingia kikamilifu katika harakati za mapambano za kutaka kuuangusha utawala dhalimu wa Mfalme Shah. Maandamano na harakati za wananchi wa Esfahan zilikuwa na umuhimu mkubwa kiasi kwamba, utawala wa Mfalme Shah uliingiwa na hofu na wahaka mkubwa hali iliyoufanya uanzishe serikali ya kijeshi mjini humo.
Na tarehe 13 Agosti miaka 115 iliyopita alizaliwa Alfred Hitchcock mtengeneza filamu mashuhuri wa Kiingereza. Alionesha kazi yake ya kwanza mwaka 1920 na baadaye akaanza kujihusisha na uongozaji filamu. Filamu zake za kuogopesha na za kusisimua zilikuwa mashuhuri mno katika zama hizo. Filamu hizo zilimfanya awe mashuhuri kwa jina la the Master of Suspense. Miongoni mwa filamu zake ni The Man Who Knew Too Much na Young and Innocent. Alfred Hitchcock aliaga dunia tarehe 28 Aprili 1980.

0 comments:

Chapisha Maoni