Ijumaa, Agosti 15, 2014

MAKUBWA MAPYA YA NDEGE ILIYOPOTEA MALAYSIA, HAYA NI MAAJABU YA KARNE!!!!

Ndege ya Malaysia Flight MH 370 iliyopotea miezi mitano iliyopita imerudi tena kwenye vichwa vya habari ikiwa na ripoti za kushangaza.
Ripoiti ya benki ya Kuala Lumpur, Malaysia inaoensha kuwa akaunti za abiria wanne wa ndege hiyo zimechukuliwa pesa July 18 mwaka huu fedha ambazo zitajwa kuwa zaidi ya £20,000.
Msaidizi wa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Malaysia, Izany Abdul Ghany ameiambia Mirror kuwa wanaendelea kufanya uchunguzi kufahamu jinsi ambavyo pesa hizo zilivyopotea.
We are investigating the case as unauthorised access with intent to commit an offence,We are getting CCTV footage from the bank to identify the suspects involved.
Ameeleza kuwa pesa hizo zilitolewa katika akaunti ya abiria watatu na kuwekwa katika akauti ya abiria wanne kabla ya kutolewa kabisa.
Ndege ya Malaysia ilipotea March 8, 2014 ikiwa imebeba wafanyakazi 12 na abiria 227 kutoka katika mataifa mbalimbali na bado haijapatikana huku maafisa wakitangaza kuwa watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo wamepoteza maisha.

0 comments:

Chapisha Maoni