Jumanne, Agosti 12, 2014

HISTORIA ZA MITAA NA BARABARA ZA DAR ES SALAAM

Nnamdi Azikiwe alikuwa ni kiongozi wa kwanza wa Nigeria mara baada ya uhuru wa nchi hiyo. Barabara yetu ile maarufu imepewa jina hilo kama kumbukumbu yake. Alifariki mwaka 1996
Hassan Omari Makunganya alikuwa kiongozi wa Wangindo. Aliongoza watu wake kupigana na Wajerumani dhidi ya utawala wa Wajerumani. Alishirikiana na akina Kinjekitile Ngwale katika vita iliyojulikana kama 

Majimaji (1905 - 1907)
mtaa wa Lindi...
Mtaa huu ndio mrefu kuliko mitaa yote hapa Dar.

Mtaa wa Agrey...
Huu ni mtaa wa pili kwa urefu Dar.

Mtaa wa Congo...
upo Kariakoo.
Huu ni mtaa ambao una pilika na Tashtiti kuliko mitaa yote Tanzania.
Halahala, Mtaa huu ukijishaua kuzubaa tu unaibiwa.

Mtaa wa Sikukuu...
Mtaa huu ni mtaa unaouza madiko diko usiku kucha.
Nenda muda wowote mtaa huu utapata Chakula.
huu pia uko Kariakoo.

Mtaa wa Chui...
Pia nao upo Kariakoo.
Ni mtaa unaoaminika kuwa na walaji Mirungi kuliko mtaa wowote Dar es Salam.

Mtaa wa Pemba...
Upo Kariakoo.
Umelaaniwa, hauna Lami.
kwa taarifa yako mtaa huu unapita katikati ya soko kuu la Kariakoo.

Mtaa wa Swahili.
Huu mtaa upo Kariakoo.
Mtaa huu unaanzia Kariakoo Shimoni unaishia Gerezani.

Mtaa wa Twiga.
Upo Kariakoo.
Ndipo lilipo jengo la club yenye mafanikio zaidi hapa nchini.
Hapa naizungumzia club ya YANGA.

Itaendelea...

0 comments:

Chapisha Maoni