Jumatatu, Julai 28, 2014

WATANZANIA WATAKIWA KUMHESHIMU RAIS KIKWETE

Watanzania wameshauriwa kuendelea kuheshimu hadhi na mamlaka aliyonayo Rais wa Jamhuri ya Muunganao wa Tanzania, Jakaya Kikwete, kwa kuthamini na kuzingatia mwongozo na ushauri mbalimbali anaoutoa kwa wananchi, kwani mamlaka hayo yanatoka kwa Mungu.
Askofu mstaafu wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Dodoma, Mhashamu Mathias Isuja, amesema hayo jana katika mahubiri yake maalumu wakati wa Misa ya Jumapili katika Parokia ya Makole, Jimbo Katoliki la Dodoma. Misa hiyo ilikuwa maalumu kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kiaskofu Jimbo la Kondoa.

Askofu Isuja, ambaye ni Askofu wa kwanza Mtanzania katika jimbo hilo, aliwataka Watanzania waombe Mungu, ili ajalie busara na hekima katika kutenda na kuamua mambo mbalimbali yahusuyo nchi, hasa kuhusu mchakato wa kupata Katiba mpya.
Alisema hafurahishwi na jinsi makundi mbalimbali ya Watanzania wanavyolumbana na kubeza hata miongozo inayotolewa na Rais Kikwete.

0 comments:

Chapisha Maoni