Jumatano, Julai 30, 2014

UZURI WA MCHEZAJI MPIRA WAZUA KIZAA ZAA UWANJANI, PICHA NA VIDEO VIKO HAPA

Kwa kawaida mashabiki wa mpira wa miguu, mpira mikono, mpira wa kikapu au hata ‘handball’ huingia kwa wingi uwanjani kushangilia mechi kati ya timu zao na wapinzani. Lakini hii imekuwa tofauti kwa mashabiki wa mpira wa Volleyball huko Taiwan.
Vyombo vya habari vya nchini humo vimeeleza kuwa wadau wa mpira wa Volleyball wamemlalamikia mchezaji wa kike mrembo na mwenye mvuto haswaa anaefahamika kwa jina la Sabina Altynbekova  kuwa chanzo cha kuharibu uhalisia na utamu wa mechi za mchezo huo pale timu yake inayoitwa ‘Kazakhstan’ inapokutana na timu nyingine.
Taarifa hizo zinaeleza kuwa umati wa mashabiki hasa wanaume wanaonekana kuwa huingia uwanjani kumuangalia zaidi msichana huyo mwenye umri wa miaka kati ya 17 na 18, na hivyo mvuto wake huharibu uhalisia wa mechi kwa kuwa kila anaposhika mpira hushangiliwa sana kama ndiye mchezaji pekee kitu ambacho kinaonekana kuwa tatizo hata kwa wachezaji wenzake.
Kocha wa timu hiyo, Nurlan Sadikov pia ameonekana kusikitishwa na hali hiyo inayoathiri saikolojia ya wachezaji wengine wa timu yake.

Haiwezekani ifanyike hivi…umati wa watu unafanya kama vile kuna mchezaji mmoja tu kwenye hii ligi hii ya mabingwa.
Kocha  Sadikov aliiambia Tengrin News.
Video ya sabina, Altynbekova iliwekwa YouTube wiki iliyopita na tayari imeshatazamwa zaidi ya 1, 153, 646.

0 comments:

Chapisha Maoni