Jumatano, Julai 02, 2014

HOSPITALI YA RUFAA MTWARA HALI MBAYA

Hospital ya rufaa ya mkoa wa Mtwara ya Ligula imelalamikiwa kwa kukosa huduma za vipimo vya damu huku wodi ya watoto wakilazimika kulala watoto wawili hadi wa tatu kitanda kimoja, kutokana na ukosefu wa vitanda.
Baadhi ya wakazi wa Mtwara waliopata huduma za matibabu kwenye hospital hiyo ya rufaa ya mkoa wa Mtwara ya Ligula wamedai,  wanapoandikiwa na daktari kwenda kupata vipimo vya damu maabara, huambiwa waende kwenye zahanati za watu binafsi na majibu ya vipimo hivyo warejeshe hospitalini hapo, kwa kuwa hospital hiyo ya rufaa haina vifaa vya kupimia damu, hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa na kuitaka serikali kuingilia kati tatizo hilo kwani linaadhiri utoaji wa huduma bora kwenye sekta hiyo ya afya.     
Alipoulizwa juu ya malalamiko hayo, kaimu mganga mfawidhi hospitali hiyo ya rufaa ya mkoa wa Mtwara ya Ligula Dr. Joseph Mwiru amekiri  tatizo hilo lilikuwepo miezi michache iliyopita na kwa sasa limepatiwa ufumbuzi, na kuhusu  wodi ya watoto kujaa na watoto  kulazimika kulala wawili hadi watatu kitanda kimoja,amesema hali hiyo  imetokana na magonjwa ya mlipuko kama Typhod, unaosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa.

0 comments:

Chapisha Maoni