Jumatatu, Julai 28, 2014

ARUSHA YAONGOZA KILIMO CHA BANGI TANZANIA

Tafiti zinaonyesha kuwa, mkoa wa Arusha unaongoza kwa kilimo haramu cha bangi ambayo imekuwa ikiharibu maisha ya vijana wengi licha ya viongozi wa mkoa huo kukemea vikali juu ya ustawishaji wa mmea huo huku wakisisitiza kula sahani moja na wahusika bila mafanikio, ambapo eneo la Kisimiri lililopo Wilayani Arumeru likitajwa kuongoza kwa kilimo hicho.
Aidha, kumekuwepo na mjadala katika mtandao wa JamiiForums kuwa Polisi mkoani humo baada ya kufanikiwa kwa kiasi fulani kunasa genge la ulipuaji mabomu, sasa limeelekeza nguvu zake katika suala la mihadarati hali iliyotajwa kuchangia kunaswa kwa magunia hayo.

0 comments:

Chapisha Maoni