Jumanne, Mei 27, 2014

WATANGAZAJI WA KIKE TANZANIA WALIOVAMIA FANI YA UTANGAZAJI

Nainukuu hii barua kutoka kwa mwandishi wa Global Publishers Joseph Shaluwa 
KWENU

Watangazaji wa kike Bongo. Poleni na kazi za kila siku na hongereni kwa namna mnavyojituma kuhakikisha gurudumu linasonga mbele.
Nimeona leo ni vyema niwakumbuke kwa barua yenye lengo la kukumbushana kuhusu weledi wa kazi yenu ya utangazaji. Nianze kwa kusema kwamba, kiukweli baadhi yenu ni kama mmevamia fani!
Heshima ya utangazaji iliyokuwepo zamani imeanza kupotea! Kuna watangazaji wanatia kinyaa. Yaani wamegeuza runinga kama mahali pa matangazo.
Mavazi ya baadhi yenu si ya staha. Nimekuwa nikitazama vipindi mbalimbali vinavyoendeshwa na wanawake, mavazi ni ya hovyo.
Kwanza yanaacha sehemu kubwa ya miili nje, lakini mbaya zaidi kuna wengine bila haya, kwenye taarifa za habari, utakuta ameacha sehemu kubwa ya matiti nje, uso ameupara kupitiliza! Ya nini yote hayo?
Kinachotakiwa ni mtangazaji kuonekana nadhifu na asome vizuri habari. Sasa hayo mambo ya kuanika matiti nje ni kwa faida ya nani?
Wanaokera zaidi ni wale ambao wanajifanya wamevaa kiheshima lakini kifuani wanapandisha matiti juu na kuyaminya ili yaonekane! Sijui ndiyo staili mpya?
Hata kama ni staili, kwenye runinga si mahali pake. Fanya hivyo nje ya runinga, siyo sehemu ambayo inafuatiliwa na watu wengi. Kwa nini usijiheshimu?
Ukiachana na habari kuna vipindi vinavyoongozwa na wanawake, baadhi yao hawana maadili, achilia mbali mavazi wanayovaa lakini hata maneno wanayotumia si ya kistaarabu.
Mnatakiwa kufahamu kuwa runinga ni chombo cha habari, ambacho kinapaswa kuheshimiwa. Watu wanaokuwa wamekaa nyuma ya runinga wanategemea kupata kitu sahihi kutoka kwenu.
Si kujianika! Hapo si mahali pa kujianika. Inafikia mahali mpaka mtu unaweza kujiuliza; hao wenye tabia hizo, wanakuwa wanatafuta nini  zaidi ya kutoa taarifa kwa jamii?
Maana isije kuwa mna yenu. Manenomaneno mengi sana kuhusu wasanii wa sanaa mbalimbali nchini. Wanaonekana kama wahuni kutokana na mavazi yao. Vipi kuhusu ninyi?
Mnatakiwa kujitambua na kuthamini utu wenu, mfahamu kuwa mmepewa dhamana kubwa ya kubeba vyombo vya habari. Ukiwa mbele ya kamera, maana yake ujue wewe ni chombo cha habari.
Lindeni maadili ya Kitanzania, msivunje miiko  ya utangazaji habari. Viongozi wa vituo mko wapi? Wekeni sheria zinazolinda maadili.
Nasisitiza, siyo wote ila wapo ambao wameingilia fani wakiwa na malengo yao vichwani mwao! Wapo wenye staha na wanaojitambua. Mfano mzuri ni Rehema Salum, Fatma Almasi Nyangasa, Grace Kingalame na wengine wengi wanaojitambua.
Wenye tabia hizo hebu jiangalieni upya.
Yuleyule, Mkweli daima, Joseph Shaluwa

0 comments:

Chapisha Maoni