Alhamisi, Mei 22, 2014

JOYCE BANDA: TARATIBU ZA UCHAGUZI ZIMEKIUKWA MALAWI

Rais wa Malawi, Joyce Banda amesema udanganyifu mkubwa umetokea kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya Jumanne na ametaka zoezi la kuhesabu kura lianze upya. Bi. Banda ambaye yumkini akapoteza cheo chake amesema miongoni mwa udanganyifu uliothibitishwa na mawakala wa chama chake ni pamoja na mtu mmoja kupiga kura zaidi ya mara mbili, wagombea fulani wa urais kupata kura nyingi zaidi zisizoendana na idadi ya wapiga kura waliojiandikisha katika baadhi ya maeneo pamoja na kudukuliwa kompyuta za tume ya uchaguzi. Hata hivyo, Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Maxon Mbendera, amekanusha madai ya kudukuliwa tarakilishi za tume hiyo akisema kilichofanyika ni mitambo kuvurugika. Mbendera amesema baada ya mitambo ya elektroniki kufeli kufanya kazi, wameamua kuhesabu kura kwa mikono na ameahidi kwamba matokeo yatatangazwa punde baada ya zoezi hilo kukamilika.

0 comments:

Chapisha Maoni