Alhamisi, Mei 29, 2014

DIAMOND AFANYIWA KITU MBAYA MAREKANI

Unaweza kudhani kuwa mambo haya yapo hapa tzee tu, kumbe ni kila sehemu, hata huko kwa States yapo, ile show aliyekuwa aifanye mkali wa Afro Pop kutoka Bongo  Diamond platnumz, imeingia dosari, baada ya promota kushindwa kufikia ahadi zake katika swala zima la mkwanja, Show hii iliyokuwa ifanyike siku ya ijumaa ya kesho tarehe 30 May mjini Northampton, ndiyo ishakufa tena baada ya Dangote kuzinguliwa kibongo bongo.
Diamond Platnumz alifunguka kupitia mtandao wa Instagram na kusema haya
Kutokana na Promoter kushindwa kutimiza makubaliano hadi sasa, imetubidi kukatisha show ya Northampton…! NEW YORK, NEW JERSEY niko njiani tukutane tare 31 ya Mwezi huu!

0 comments:

Chapisha Maoni