Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amekadhibisha vikali tuhuma
zilizoelekezwa dhidi yake kwamba anasambaza silaha kwa wananchi wa nchi
hiyo. Rais Nkurunziza ameyasema hayo baada ya kukutana na Balozi wa
Marekani mjini Bujumbura. Rais Nkurunziza amesisitiza kwamba zoezi la
kuifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo halitafanyika. Naye Willy
Nyamitwe Msemaji wa Rais Nkurunziza amesema kuwa, habari zilizoenezwa
kwamba Rais Nkurunziza anasambaza silaha kwa wananchi hazina ukweli
wowote na zimetolewa kwa shabaha ya kuzichochea fikra za walio wengi
nchini humo. Nyamitwe amesema kuwa Burundi itaitisha uchaguzi huru na wa
haki kwa kutegemea katiba iliyopo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, tarehe
21 Machi, Bunge la Burundi lilitupilia mbali mpango wa serikali wa
kuifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo.
0 comments:
Chapisha Maoni