Ijumaa, Machi 14, 2014

MOURINHO AMKOROMEA TOURE


Jose Mourinho amejibu kauli ya Yaya Toure aliyedai kuwa meneja huyo wa Chelsea hakuonyesha heshima kwa timu nyingine za Uingereza kwa kuzungumza wazi kuhusu matumaini yao katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya wiki iliyopita.
Toure ambaye alikuwemo katika kikosi cha Manchester City kilichopoteza dhidi ya Barcelona siku moja baada ya Arsenal kutolewa na Bayern Munich,alionekana kutofurahishwa na maneno ya Mourinho lakini akiongea kuelekea mchezo
wa ligi dhidi ya Aston Villa,alisema kuwa maneno yake yalikuwa na lengo la kuonyesha ushirikiano pekee.
Huku akisisitiza kuwa,”Kama kusema kabla ya michezo ya Munich na Camp Nou kuwa michezo hii bado haijaisha kwani Arsenal na Man City wanauwezo na ubora wa kwenda huko ugenini na kubadilisha mambo,kama kuonyesha kwangu ushirikiano kwa timu ambazo zinatoka nchi ambayo nafanya kazi inachukuliwa kama sio heshima,sawa basi hiyo sio heshima.”

0 comments:

Chapisha Maoni