Shirika la Misaada la “Save the Children” limeonya kuwa mfumo
wa kiafya wa Syria uko katika hali ya kusambaratika na kwamba watoto
wadogo wanataabika kutokana na kukosekana huduma za afya zinazohitajika.
Shirika hilo la hisani limesema katika ripoti yake ya jana kuwa,
karibu asilimia 60 ya hospitali huko Syria zimebomolewa au kuharibiwa
tangu kuzuka machafuko nchini humo miaka mitatu iliyopita na kwamba
karibu nusu ya madaktari wameikimbia nchi hiyo.
Shirika la hisani la “Save the Children” limekutaja kusambaratika kwa
mfumo wa afya wa Syria kuwa ni jambo la kutisha na kuongeza kuwa idadi
ndogo ya wafanyakazi wa sekta hiyo wanahangaika kuwahudumia raia
wanaojeruhiwa kutokana na machafuko yanayoendelea nchini humo.




0 comments:
Chapisha Maoni