Ubalozi wa Tanzania nchini Rwanda umeeleza kusikitishwa na taarifa za
blog ya Rwanda “News of Rwanda” ambayo inaunga mkono serikali ya nchi
hiyo iliyotolewa mwishoni mwa juma zikimtuhumu rais wa Tanzania Jakaya
Kikwete kwa kuunga mkono na kufanya mikutano na wanachama wa makundi ya
waasi yanayopingana na serikali ya Rwanda.
Akizungumza na Sauti ya Amerika mkurugenzi wa mawasiliano ya Ikulu ya
Tanzania Salva Rweyemamu amesema wao wameshangazwa kwa sababu mwaka
jana kulikuwa na matatizo na marais wa nchi hizo wameshazungumza
vizuri wakakubaliana na kuonyesha kwamba sasa mambo yameisha na kwamba
wanaendeleza urafiki wao, udugu wao na ujirani mwema wa miaka mingi kati
yao na kuongeza kwamba hilo ni jambo la kusikitisha sana kwa upande wa
Tanzania.
Akizungumza na Sauti ya Amerika mkurugenzi wa mawasiliano ya Ikulu ya
Tanzania Salva Rweyemamu amesema wao wameshangazwa kwa sababu mwaka
jana kulikuwa na matatizo na marais wa nchi hizo wameshazungumza
vizuri wakakubaliana na kuonyesha kwamba sasa mambo yameisha na kwamba
wanaendeleza urafiki wao, udugu wao na ujirani mwema wa miaka mingi kati
yao na kuongeza kwamba hilo ni jambo la kusikitisha sana kwa upande wa
Tanzania.
Ametoa wito kwa vyombo vya habari nchini humo visaidie kujenga
uhusiano mwema na visiwe mwanzo wa choko choko ya kugombanisha watu
akiuliza kuwa “Tanzania wakigombana na Rwanda magazeti yatauzwa?” au
mkiwa kwenye hali ya vurugu kama ilivyo nchi zingine ambapo watu
wanapigana kila siku kuna watu wananunua magazeti pale?



0 comments:
Chapisha Maoni