Kwa mujibu wa chanzo kingine cha habari, Wastara alitaka kukatisha
uhai wake kutokana na kuchoka kunyanyapaliwa, kudhalilishwa na
kutongozwa mara kwa mara na wanaume, hali ambayo imekuwa ikimfedhehesha
mbele ya jamii.
Chanzo hicho kimesema kwamba kabla ya tukio hilo, Wastara alikuwa
akilalamika kudhalilishwa na watu anaowadai fedha zake ambao hawataki
kumlipa haki yake.
“Kuna watu wengi ambao Wastara anawadai lakini wanamsumbua kwa kumuona ni mwanamke asiye na nguvu na wengine wanatumia mwanya huo kumtongoza, mwenyewe anaamini haya yote yanatokea kwa kuwa Sajuki hayupo,” kimetoboa chanzo hicho.
“Kuna watu wengi ambao Wastara anawadai lakini wanamsumbua kwa kumuona ni mwanamke asiye na nguvu na wengine wanatumia mwanya huo kumtongoza, mwenyewe anaamini haya yote yanatokea kwa kuwa Sajuki hayupo,” kimetoboa chanzo hicho.
Habari zaidi zinadai kwamba hivi sasa Amanda anaendelea kumwekea
ulinzi wa karibu Wastara ili asiweze kuchukua uamuzi mbaya wa kukatisha
maisha yake.
Baada ya kuyapata madai hayo, mwandishi wetu alimpigia simu Wastara ili kupata undani wa tukio hilo lakini kwa muda mrefu simu yake ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa.
Baada ya kuyapata madai hayo, mwandishi wetu alimpigia simu Wastara ili kupata undani wa tukio hilo lakini kwa muda mrefu simu yake ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa.
Amanda alitafutwa ili kuweza
kupata ukweli wa madai hayo na kumuuliza kama bado yupo kwa Wastara.




0 comments:
Chapisha Maoni