Jumapili, Machi 12, 2017

UKINUNUA iPHONE 7 CHINA UMEJIFUKUZISHA KAZI

Kampuni kadha nchini Uchina zimetoa onyo kali kwa wafanyakazi wake na kuwataka wasinunue simu mpya ya kampuni ya Apple, iPhone 7.
Kampuni zilizotoa marufuku hiyo zinasema ni kwa sababu za kizalendo.
Nyingine zimesema zinataka kuwafunza wafanyakazi wake kutopenda sana raha na anasa za dunia.
Kampuni ya dawa ya Nanyang Yongkang Medicine, katika mkoa wa Henan, ni moja ya zilizoagiza wafanyakazi wake kutonunua simu za iPhone 7 au Iphone 7 Plus.
"Ukivunja agizo hili, njoo moja kwa moja hadi afisini na utukabidhi barua yako ya kuacha kazi," ilani kutoka kwa kampuni hiyo iliyotumwa kwa wafanyakazi inasema.

0 comments:

Chapisha Maoni