Jumamosi, Julai 05, 2014

TETESI ZA USAJILI ULAYA

Mabingwa wa EPL Manchester City wanafikiria kumchukua kiungo wa Everton Ross Barkley kwa pauni milioni 25 (Daily Mirror), boss wa West Ham Sam Allardyce anafikiria kupanda dau kumchukua mshambuliaji wa kimataifa wa Ecuador Enner Valencia aliyepachika mabao matatu katika Kombe la Dunia (Daily Star), Liverpool wanataka kumchukua beki wa Seattle Sounders, DeAndre Yedlin, na huenda wakamualika kwa majaribio katika mechi za kabla ya kuanza msimu (Metro), Barcelona bado hawajafikia makubaliano na Liverpool kuhusiana na uhamisho wa Luis Suarez, mkataba huo hautarajiwi sasa kuafikiwa hadi wiki ijayo (Guardian), beki wa zamani wa Chelsea Ashley Cole anafanya mazungumzo na klabu ya Roma ya Italia kusaini mkataba wa miaka miwili (Daily Mail), Tottenham na Arsenal zote zinamfuatilia beki wa kati wa Uholanzi Joel Veltman (Daily Mirror), mshambuliaji wa Uholanzi Klaas-Jan Huntelaar amesema atazungumza na Schalke kwanza baada ya kuhusishwa na klabu ya Liverpool (Evening Standard), beki mwingine wa Uholanzi Daryl Janmaat ananyatiwa na Newcastle na Manchester United (Daily Mail), kiungo Mfaransa anayechezea Southampton, Morgan Schneiderlin ana uhakika wa kuondoka na amewaambia wenzake kuwa hatorejea baada ya Kombe la Dunia (Daily Star), QPR wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Eduardo (Daily Star), Chelsea wamefanya jaribio la kumsajili kiungo wa Bayern Munich, Toni Kroos, ambaye pia anasakwa na Real Madrid (Daily Star), meneja wa Arsenal, Arsene Wenger atamtoa Joel Campbell kwa mkopo kwa msimu ujao. West Ham, Everton, Southampton na Newcastle zote zinamtaka (Daily Mail), Alexis Sanchez amekatisha likizo yake ili kutatua hatma yake Barcelona. Juventus na Arsenal wamewasilisha maombi yao. Arsene Wenger ametoa dau la kuvutia zaidi (AS), Arsenal na Southampton zote zinamuwanja beki wa kushoto wa Colombia Pablo Armero (ESPN), Chelsea wametoa pauni milioni 11.8 kumsajili beki wa kushoto wa Atlètico Madrid, Filipe Luis, lakini klabu hiyo inataka milioni 19(Marca). Share tetesi na wapenda soka.

0 comments:

Chapisha Maoni