Jumatano, Aprili 23, 2014

SERIKALI YAINGILIA KATI MAFANIKIO YA TIMU YA MBEYA CITY

Moto umeanza kuwaka kwa Halmashauri ya Mkoa wa Mbeya kwa kuwataka watu kuacha tabia ya kufanya siasa kwa timu ya Mbeya City ili kuifanya timu hiyo kuendelea kuwa na uhai.
Mbeya City imefanikiwa kumaliza Ligi ya Tanzania Bara huku ikishika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, huku Azam FC ikinyakua taji hilo na Yanga SC kushika nafasi ya pili.
Kwa mujibu wa wadau wa soka mkoani Mbeya, watu wameanza kujipitisha wakijinadi kuwa timu hiyo imefanikiwa kwa uwezo wao, wakati ni juhudi za Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Katibu Tawala wa mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja, alizungumzia hilo kwenye hafla ya kuwapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu ya Mbeya City.
Timu hiyo sasa imevunja kambi yao baada ya ligi kumalizika na kuiweka timu katika mazingira mazuri ya kushiriki ligi ijayo kwa mafanikio.
Baadhi ya wanasiasa mkoani hapa wameanza kuyahusisha mafanikio ya timu hiyo na harakati zao za kisiasa za vyama vyao hali ambayo ni hatari kwa uhai wa Mbeya City katika ulimwengu wa soka nchini, maana huu sio mwendo mzuri.
Siasa wakati mwingine inaweza kuwagawa mashabiki wa timu hiyo kutokana na kwamba kila mmoja ana mapenzi na chama chake
 alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mbeya City, Musa Mapunda, alisema baada ya kufanikiwa kushika nafasi ya tatu msimu huu, sasa wanaweka mikakati ya kuhakikisha timu hiyo inachukua ubingwa wa ligi Kuu ya Soka Tanzania bara msimu ujao.
Naye kocha Mkuu wa timu hiyo, Juma Mwambusi, alisema vijana wake wamefanya kazi nzuri na watajiandaa vyema kwa ligi ijayo.
Mbeya City ilianzishwa Julai mwaka 2011 na huu ni msimu wake wa kwanza kushiriki ligi hiyo na kupata mafanikio yak upigiwa mfano.

0 comments:

Chapisha Maoni